Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kurugenzi ya Udhibiti Ubora na Masoko

Majukumu

Kurugenzi inatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kumshauri Mkurugenzi Mkuu katika masuala yote yanayohusu ubora na masoko ya tumbaku;
  • Kuwasiliana na nchi nyingine za kigeni zinazozalisha tumbaku kama nguvu ya pamoja ya kujadiliana bei katika meza ya mazungumzo;
  • Kusimamia shughuli za utangazaji wa tumbaku ndani na nje ya nchi;
  • Kuratibu, kudhibiti na kutathmini masoko ya tumbaku ikiwa ni pamoja na utafiti na huduma za ugani;
  • Kupanga, kuratibu, na kusimamia utafiti wa masoko na utaratibu wa uuzaji wa tumbaku mbichi;
  • Kutunga sheria na kanuni za udhibiti na uhakiki wa ubora; na
  • Kusimamia uzingatiaji wa sheria na kanuni zinazosimamia tasnia ya tumbaku katika masoko katika ngazi zote.