Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kitengo cha Huduma za Sheria

Majukumu

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kutafsiri nyaraka za kisheria na kuishauri Bodi;
  • Kuidhinisha nyaraka za kisheria za Bodi;
  • Kupitia hati za Udhamini, mikataba ya makubaliano, mikataba na nyaraka nyingine za kisheria;
  • Kutayarisha maelezo ya kisheria na kuiwakilisha Bodi katika mashauri ya kisheria;
  • Kuwasiliana na Wakala wa kisheria wa nje katika masuala ya kisheria na kushiriki au kuendesha mashauri ya Bodi;
  • Kupitia na kuandaa marekebisho ya Sheria ya Sekta ya Tumbaku na kanuni zake;
  • Kudumisha ulinzi salama wa nyaraka za kisheria za Bodi;
  • Kupanga na kuitisha kikao cha Bodi ya Wakurugenzi;
  • Kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya vikao vya Bodi ya Wakurugenzi;
  • Kuwa Katibu wa vikao vya Uongozi wa Bodi; na
  • Kuandika kumbukumbu wakati wa vikao vya Bodi ya Wakurugenzi na vile vya Uongozi wa Bodi.