Kitengo cha Huduma za Sheria
Majukumu
Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:
- Kutafsiri nyaraka za kisheria na kuishauri Bodi;
- Kuidhinisha nyaraka za kisheria za Bodi;
- Kupitia hati za Udhamini, mikataba ya makubaliano, mikataba na nyaraka nyingine za kisheria;
- Kutayarisha maelezo ya kisheria na kuiwakilisha Bodi katika mashauri ya kisheria;
- Kuwasiliana na Wakala wa kisheria wa nje katika masuala ya kisheria na kushiriki au kuendesha mashauri ya Bodi;
- Kupitia na kuandaa marekebisho ya Sheria ya Sekta ya Tumbaku na kanuni zake;
- Kudumisha ulinzi salama wa nyaraka za kisheria za Bodi;
- Kupanga na kuitisha kikao cha Bodi ya Wakurugenzi;
- Kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya vikao vya Bodi ya Wakurugenzi;
- Kuwa Katibu wa vikao vya Uongozi wa Bodi; na
- Kuandika kumbukumbu wakati wa vikao vya Bodi ya Wakurugenzi na vile vya Uongozi wa Bodi.