Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kurugenzi ya Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala

Majukumu

Kurugenzi inatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kumshauri Mkurugenzi Mkuu katika masuala yanayohusu utawala na Mipango na Maendeleo ya Rasilimali Watu;
  • Kusimamia kumbukumbu sahihi za rasilimali watu;
  • Kusimamia utayarishaji na utekelezaji wa Bajeti ya Mishahara (PE);
  • Kusimamia utayarishaji wa taarifa za Rasilimali watu na utawala;
  • Kusimamia ajira, uteuzi na upandishaji vyeo kwa wafanyakazi wa Bodi;
  • Kusimamia uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Nyaraka za Kiutumishi;
  • Kusimamia mikataba ya watoa huduma;
  • Kusimamia majengo ya ofisi, vifaa na matengenezo yake;
  • Kuhakikisha kuwa makato ya kisheria ya wafanyakazi yanalipwa.
  • Kusimamia ustawi wa wafanyakazi (ujira, mishahara na marupurupu mengine);
  • Kusimamia Tathmini ya Mahitaji ya Mafunzo na maandalizi ya Mpango wa Mafunzo.