Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kurugenzi ya Fedha

Majukumu

Kurugenzi inatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kumshauri Mkurugenzi Mkuu katika masuala yanayohusu Mipango na Usimamizi wa Fedha na matumizi ya Bodi;
  • Kusimamia uendeshaji wa shughuli za kifedha za Bodi;
  • Kuimarisha usimamizi wa fedha na hesabu;
  • Kufanya majumuisho ya bajeti ya mwaka ya Bodi ya matumizi (OC) na Mishahara (PE);
  • Kuelekeza na kusimamia utayarishaji wa taarifa za fedha za mara kwa mara;
  • Kuimarisha matumizi bora ya mapato ya Bodi katika ununuzi na utoaji wa huduma na vifaa;
  • Kufuatilia upatikanaji wa fedha kutoka katika vyombo husika na kusimamia bajeti ya matumizi ya Bodi na kila idara; na
  • Kuwezesha ukaguzi wa taarifa za fedha za Bodi.