Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
Majukumu
Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:
- Kufuatilia na kupitia taratibu na udhibiti wa uendeshaji wa Bodi;
- Kushauri juu ya utekelezaji wa taarifa ya Mkaguzi wa Nje;
- Kusimamia utayarishaji wa taarifa za ukaguzi wa ndani;
- Kuandaa na kubuni taratibu/mifumo ya ukaguzi;
- Kufanya mapitio ya sera za udhibiti wa ndani ili kuhakikisha utekelezaji mzuri wa bajeti;
- Kusimamia uzingatiaji wa Kanuni za Fedha na Utumishi;
- Kusimamia ukaguzi wa ndani wa mara kwa mara na maalum; na
- Kuwezesha Ukaguzi wa Nje.