Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani

Majukumu

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kufuatilia na kupitia taratibu na udhibiti wa uendeshaji wa Bodi;
  • Kushauri juu ya utekelezaji wa taarifa ya Mkaguzi wa Nje;
  • Kusimamia utayarishaji wa taarifa za ukaguzi wa ndani;
  • Kuandaa na kubuni taratibu/mifumo ya ukaguzi;
  • Kufanya mapitio ya sera za udhibiti wa ndani ili kuhakikisha utekelezaji mzuri wa bajeti;
  • Kusimamia uzingatiaji wa Kanuni za Fedha na Utumishi;
  • Kusimamia ukaguzi wa ndani wa mara kwa mara na maalum; na
  • Kuwezesha Ukaguzi wa Nje.